Ukatili wa polisi marekeni dhidi ya watu weusi waendelea

Ukatili wa polisi US dhidi ya watu weusi waendelea
Vitendo vya ukatili na ukandamizaji wa polisi dhidi ya raia wa Marekani wenye asili ya Kiafrika vingali vinaendelea. Jana kulisambazwa video mpya ya ukatili wa polisi dhidi ya kijana mwengine mwenye asili ya Kiafrika huko New York, Marekani, ambayo inamuonyesha kijana huyo akipigwa vikali na kutukanwa na polisi na kisha kukandamizwa ardhini. 
Kwa mujibu wa video hiyo, kijana huyo anayefahamika kwa jina la Hamer na anayedhaniwa kuwa na umri wa miaka 17, alishambuliwa na polisi kwa kisingizio cha kuvuta bangi. Habari zinasema kuwa, licha ya kijana huyo kufanyiwa ukatili huo bila ya kuwa na utetezi wowote na yeye kuishia kupiga kelele za kuomba msaada, lakini alikutwa akivuta sigara ya kawaida tu kinyume na madai ya polisi kuwa alikuwa akivuta bangi. 
Wazazi wa kijana huyo wamesema kuwa kijana wao amepata matatizo katika ubongo wake kutokana na kipigo kikali alichokipata kiasi kwamba hawezi tena kufanya kazi yoyote yeye mwenyewe bila ya msaada. Hii ni katika hali ambayo hivi karibuni pia, kulisambazwa video iliyomuonyesha polisi wa Marekani wakimuadhibu vikali raia mwengine mwenye asili ya Kiafrika kwa kosa la eti kuendesha gari bila kuvaa mkanda.-Iran



Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4