Pluijm, Mkwasa wachemka Saudi Arabia


MAKOCHA wa zamani wa Yanga, Mholanzi Hans Van Der Pluijm na Boniface Mkwasa, wamekatisha mikataba yao na klabu ya Al Shoalah FC ya Ligi Kuu Saudi Arabia baada ya klabu hiyo kuwalazimisha kwa kuwasajilia wachezaji wasiokuwa na viwango huku matatizo ya kifedha na kiongozi yakiathiri maendeleo ya uwanjani.
Pluijm alisema: “Kwa bahati mbaya mambo hayakuenda vizuri. Ni kinyume na tulivyotarajia. Mimi  na kocha Mkwasa, tumefundisha klabu hiyo kwa takribani wiki tatu na sasa tumeamua kuachana nayo kwa sababu ya matatizo ya uongozi na kifedha yanayoikumba klabu hiyo.Matatizo hayo yalikuwepo toka mwanzoni tulivyowasili kwenye hiyo klabu.”
Pluijm pia alisema kuwa walikuwa na mahusiano na wakati mzuri na wachezaji na kwamba walikuwa na furaha kwa kupata mafunzo yao.
“Wachezaji walikuwa wakituamini na kupenda jinsi tulivyokuwa tukiwafundisha,  walikuwa wakitueleza kuwa wanaona mambo yamebadilika tangu tulipowasili,” alisema.
Naye Mkwasa aliyekuwa Kocha Msaidizi alisema: “Walituletea wachezaji wa ligi daraja la tatu ili tuwatumie kwa ajili ya ligi kuu. Wachezaji hao hawakuwa na viwango na hivyo viongozi wa timu walidai kutoridhika na ushirikiano wetu kwao na wakalazimu kuvunja mikataba yetu.
“Sisi ni makocha wa kimataifa, hatufanyi kazi kwa kubabaisha.”-MWANASPORT

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4