Hatimaye Rodriguez apokea tuzo


Hatimaye James Rodriguez ametuzwa tuzo la mfungaji bora.
Hatimaye mshambulzi wa Colombia James Rodriguez aliyeduwaza ulimwengu kwa kufunga mabao mengi zaidi katika kombe la dunia lililokamilika huko Brazil mwezi uliopita amepokea tuzo lake la mfungaji mabao mengi '' Golden Boot''.
Rodriguez ambaye aliyetikisa wavu mara 6 huko Brazil sasa anakibarua cha kutafuta namba huko Real Madrid dhidi ya wakinzani wenye haiba yake kama mchezaji bora msimu huu Christiano Ronaldo.
Rodriguez alinunuliwa na mabingwa hao wa kombe la mabingwa barani ulaya kutoka Monaco kwa pauni milioni 71.
Mshambulizi huyo mwenye umri wa miaka 23 alisema kuwa anamatumaini makubwa ya kutamba Santiago Bernabéu

Maoni

Machapisho maarufu kutoka blogu hii

HADITHI:MWALIMU MAGDALENA sehemu ya 1

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 5

Hadithi: Mwalimu Magdalena sehemu ya 4